<p>Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.<br>
<em><strong>2 </strong></em>Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.<br>
<em><strong>3 </strong></em>Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.<br>
<em><strong>4 </strong></em>Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.<br>
<em><strong>5 </strong></em>Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.<br>
<em><strong>6 </strong></em>Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.</p>